Home | Vacancies and Tenders | Join our mailing list | Webmail | CSO Directory | FCS Forum       ENGLISH‹›SWAHILI
..enabling effective engagement in poverty reduction efforts!
What they Say About Us
  • About Us
  • Grants
  • Services
  • Reports & Plans
  • publications
  • contact us
   
 
Download
  • Grants Application Guide - 2013 English Version
  • Mwongozo Wa Kushiriki Maombi Ya Tuzo Ya Asasi Bora...
  • Fomu Ya Maombi Ya Tuzo Ya Asasi Bora 2013
  • Mwongozo Wa Uombaji Ruzuku Mwaka 2012
  • Tuzo Ya Asasi Bora
  • More »
    Useful Links
  • Others
  • Regional and global civil society networks
  • National civil society networks and organizations
  • CSO Directory
  • cso websites funded by fcs
  • Tanzania women Teachers Association
  • Morogoro paralegal Centre
  • Christian Council Of Tanzania
  • Guluka Kwalala Youth Environmental Group
  • More »
    Your Comments
    Do you have questions/comments?
    Let us know below

    Name
    E-mail
    Comment
     
    FCS Forum Login Feedback
    Recent Topics
    Title Views Last Updated
    FCS found a different ways of publishing its reports 8 05/07/2012
    Hacked 10 12/06/2011
    NINI MTIZAMO WAKO KUHUSU BIASHARA NA SIASA? 1 26/08/2010
    NINI KINAFUATA ZANZIBAR? 2 12/08/2010
    Asasi za kiraia zina mchango gani katika kipindi hiki cha uchaguzi mkuu? 0 12/08/2010
    Top Contributors
    Lina   [ 1 ]
    Kelvin   [ 2 ]
    Noel   [ 1 ]
    James   [ 1 ]
    Hermengild Mayunga   [ 2 ]
    Michael Mpombo, KILI CENTRE, MOSHI.   [ 1 ]
    Recent Comments
    Comment User name Posted On
    we were hacked but the website is now back to its swing - other details will be uploaded Phesto Namayala 15/11/2012
    the links above are not click-able you may try below links below http://anrepeng.thefoundation-tz.org http://anrepswa.thefoundation-tz.org http://qnewsleng.thefoundation-tz.org http://qnewslswa.thefoundation-tz.org admin 25/09/2012
    Nimekuwa nikitafakari kwa kina na kwa siku nyingi sana bila kupata majibu kwa nini walemavu tunatengwa katika kufanya maamuzi? Kwa mfano hapa kwetu Tanzania walemavu wanashughulikiwa na wizara ya afya na ustawi wa jamii chini ya idara ya ustawi wa jamii ambayo ofisi zake ziko pale akiba ghorofa ya tano huku wakishughulikia walemavu wa aina zote yaani hata wale waendao kwa baisikeli swali la masingi wanafikaje kule juu ili wasikilizwe? Licha ya kuwa idara hii ndiyo inayoangalia ustwi wetu na wa wale wasiojiweza lakini ofisi zake zinaishia ngazi ya wilaya tu na hii ni kwa baadhi ya wilaya hapa nchini. Wkati watu hawa wakiwa ngazi ya wilaya lakini maafisa maendeleo ya jamii wapo hadi ngazi ya kata jamani hivi serikali hii inakusudia kumkomboa mlemavu? Siku ya Ijumaa katika kipindi cha this week in perspect nilimsikia Mh Chilgati akielezea juu ya mabadiriko kadhaa yaliyofanywa na chama tawala kwenye katiba yake lakini hata katika viti maalum vya wajumbe wa nec na mkutano mkuu hakuna nafasi ya watu wenye ulemavu licha ya kuwa kuna nafasi ya vinaja, wabunge na wazazi hivi mnadhani sisi ni wageni wa nani hapa Tanzania? Hata hivyo ilani ya chama kinachoongoza nchi hakuna mahali ambapo watu wenye ulemavu wametajwa moja kwa moja kwamba watafanyiwa hivi. Swali mnadhani kuwatendea watu wenye ulemeavu namna hii ni haki? Ni wilaya gani hapa nchini ambayo imewahi kutenga katika bajeti yake sherehe ya watu wenye ulemavu duniani ambayo huazimishwa tarehe 3/12 kila mwaka? Mbona mambo mengine hutengewa vifungu?. Wakati sasa umefika kwa wana AZAKi kutusaidia kufikisha ujumbe sisi watu wenye ulemavu ili serikali isikie na ichukue hatua. WALEMAVU KUTENGWA KATIKA VYOMBO MBALIMBALI VYA MAAMUZI 27/02/2012
    asdasdd dgsdff 08/02/2012
    Biashara ifanywe na wafanyabiashara na siasa ifanywe na wanasiasa ili kuondoa mgongano wa kimaslahi na hivyo kupunguza mianya ya rushwa ambayo ndio kansa inayoiua Taifa letu. Wanasiasa wa sasa waamue aidha wawe kwenye siasa au wawe kwenye biashara. Hii ni pamoja na nafasi kubwa katika chama, wafanyabiashara wasiruhusiwe kuingia humo kwani ni mapango yao ya kuboresha zaidi biashara zao kuliko kulitumiakia taifa. Asante Lemburis Kivuyo 25/11/2011
    Greetings, Are you working in HIV Prevention? Are you familiar with an institution, organization, group or individual working in this area? We are delighted if the answer is yes. Please help us to communicate the following information. Connect African Development Blog (http://connectafricandev.blogspot.com/) is conducting a research exercise to document EXPERIENCES, CHALLENGES and PRACTICES in HIV Prevention Efforts targeting young people. We believe there is a need to assess our position. Young people today are not the same everyday. The practices we develop, the challenges we face and the experiences have today in efforts to mitigate the pandemic will not be the same 5 years from now. That is the case for much of the thinking, the information we use to debate the issue and inform our efforts. We need to examine the picture and confirm whether we are still following the correct path of action or whether we need to change direction with new thinking and new methodology and strategies to conduct our prevention efforts. It is to this end that we invite you to contribute in an Online Information Gathering Survey. Please CLICK HERE - http://www.surveymonkey.com/s/SQMXWTJ to access the Survey Page and within 10 to 20 minutes, you should be finished. If you do not have the information to respond to the survey at hand, we encourage you to read through the questions so that you can prepare the information and you will always be able to go back to this email for the link. For more information on our thinking behind this process, please read the article "Experiences - Challenges - Approaches; where are we with HIV Prevention among young people?", which is also published on our Blog. We thank you and look forward to reading information on your experiences, challenges and practices. PLEASE HELP US TO CIRCULATE THIS TO YOUR NETWORKS. We are sorry for any cross posting. Regards, Robert Kasenene Editorial Team CAD Blog Tanzania info.codetz@gmail.com Robert Kasenene 14/11/2011
    Nionavyo mimi ni kuwa mabadiriko yanayotokea Zanzibar ni matokea ya Sera za Mheshimiwa Rais Kikwete kwani tokea awali aliazimia kuondoa mpasuko wa kisiasa Zanzibar. Hivyo matokea ya Kura ya maoni ya Zanzibar ni kuleta usalama na amani kwa Wazanzibar wote na uchaguzi wa safari hii tunategemea utakuwa huru na wa haki vinginevyo kutakuwa na unafiki ndani yake. RAJAB KABAVAKO 25/08/2010
    Jukumu la AZAKI katika kipindi hiki cha uchaguzi ni kama ifuatavyo: 1. kutokupendelea chama chochote cha siasa kwani vinginevyo zitapoteza uelekea na kusababisha vurugu. 2. kutoa elimu ya uraia na upigaji kura kwa Watanzania. Kwamba kila mtu lazima achague kiongozi amtakaye 3. kuwa waangalizi wa ndani wa uchaguzi na kuwa tayari kusema ukweli kwa kila kinachotokea katika kipindi hiki cha uchaguzi bila kufumbia macho maovu hata kama yatafanywa na chama tawala. RAJAB KABAVAKO 25/08/2010
    Mimi ninaamini kuwa mafunzo ya kujenga uzoefu wa kazi kwa wanafunzi ni mazuri na ni njia sahihi ya kumuandaa kijana kuwajibika vizuri katika maeneo yake ya kazi. kwani iwapo atakutana na wachapa kazi akafanya nao kazi, atawaiga uchapaji kazi wao lakini bahati mbaya kama akikutana na watu wavivu na wachoyo anaweza kutoka bila kujua kitu, hapa tatizo si mfumo bali watu waliomuandaa ndio wabaya. RAJAB KABAVAKO 25/08/2010
    Yanayotokea Zanzibar kwa sasa ni mema sana na kwa manufaa ya kisiasa na utulivu wa nchi. Hata hivyo, mchakato wa kura ya maoni ya kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa na mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, nayaona yanaenda kinyume na Utawala wa Sheria. Nasema hivi kwa kuwa, kuna mambo ya msingi ambayo nadhani yangepaswa kujadiliwa na Muungano, kwani tunajua fika kuwa Zanzibar si dola, japo mabadiliko hayo yameifaya/kuitamka kuwa ni dola (nchi huru). Shirika langu linakusudia (siku za usoni) kuandaa mjadala mkubwa wa wazi juu wa hali ya kisiasa ya Zanzibar kwa sasa kufuatia mabadiliko haya makubwa. Rodrick Maro 20/08/2010
    Kwa maoni yangu AZAKI nyingi zimekuwa kimya sana kwa zile zilizojaribu kutoa mwelekeo hazikufanya kwa kina na kwa mwelekeo uliopasika. Kuna mambo mengi yamejitokeza kuelekea uchaguzi mkuu yanayopingana na maadili ya Democrasia Asasi nyingi zimekuwa kimya. Rushwa ukiukwaji wa haki za kupata viongozi wenye maadili zimekuwa kimya kukemea kwa uwazi. kuonyesha mwelekeo angalao wa kuwapa wananchi wa kawaida kujua kiongozi anayetakiwa ni yupi. Zimekuwa kimya. Wataalamu wa Kikatoliki walipotoa Nyaraka mbalimbali za kutoa mwelekeo wa angalao ni kiongozi gani Tanzania tunamtaka na Serikali na viongozi wa siasa walikemea sana ASASI zilikaa kimya chache sana zilijitokeza angalao kuunga mkono na nyingine kupinga. zilizopinga hazikutoa mbadala wake. kwa maoni yangu Asasi za kiraia zinatakiwa ziamke na kuonyesha mwelekeo. Tuamke tuseme hawa hawatufai na tutoe sababu za kutofaa kwao na nini tunataka kwa maslahi ya Tanzania. Fortunatus Fungatwende 19/08/2010
    Hi, Ushauri wangu ni kuwa ni kitu kizuri kuwapa fursa watanzania wenzetu vijana kupata uzoefu. Tatizo soko wameliaribu wenyewe mara nyingi hawana utulivu na umakini wa kazi wanafikiri fursa wanazopewa ni mahali pa kufanya mchezo mchezo vi excuse vya kutohudhuria mara kwa mara na wakati mwingine hawaji. Kwa ufupi nidhamu ni shida. Ni vema anayewachukua aliweke wazi hilo. Pia hata chuo chenyewe kupitia waalimu wanaowasimamia ni tatizo. Hata wakipewa mrejeso juu ya mapungufu ya wananfunzi wao hawalifanyii kazi tatizo hilo na nilichogundua PT aiwei attached kwnye maksi za wanafunzi japo wanataka CSO ijaze form fulani. Na kama vile haitoshi pamoja na kuwapa angalizo kwa maandishi na kutojibu, mwaka unaofuata kama vile hawajui au wanadhani umesahau wanakuja tena na barua ya kuomba fursa tena na walimu wale wale wasiokuja kuwapitia wala kufanyia kazi changamoto. Mimi bado nadhani kama mzalendo ni fursa nzuri lakini ili msije shangaa mwisho wa siku kuwa kero badala ya faida ni vema kuwepo makubaliano na idara husika kuhsu ufuatiliaji, kusughulikia changamotona pia wanafunzi kupewa code of conduct na hasiye abide afukuzwe kwani kila upande unahitaji mwenzie na hivyo dhana ya kuwa anayefaidika ni asasi isiwepo. Ila nataka kusifi idara ambazo kwao mpaka wana ofisi inayoshughulikia placement za wanfunzi-engeneering-hsipoenda ulikopangiwa na husipohudhuria hawakusemeshi utakuta katika matoke yako anscond ata kama ni mwaka wa nne kumbe mwalimu alipoenda pale hakukukuta na alipewa taarifa hakuseshi anakupa maksi unazostahili utajiju ukijikuta ume disco mwisho wa siku. Ila pia nasi wana CSO. Kuna baadhi yetu wanacukua hawa vijana hakuna job description anakuja fanya nini hakuna hata on job training ya kazi iliyomleta mtu akiamka asubui leo anamtuma hiki kesho kile kaa kibarua mwisho wa kukaa hapo hawezi sema nilijifunza nini. Nadhani kama tunapenda kuwaheshimu wenzetu pamoja na ujuzi wao kidogo tuwatendee haki kwa kujiandaa na kuwaandalia cha kufanya na kuwapa fursa ya kujifunza kazi si kutumwa tumwa kusikomjenga mtu kitaaluma na kikazi Kwa nia njema fursa hii tuichangamkie kwa kuweka mazingira mazuri kila upande unufaike WISE 13/07/2010
    Sisi Wafanyakazi wa ASIZE (NGOs) za Kitaifa na Kimataifa tunahitaji kuwa na umoja wetu wa wafanyakazi kwa sababu kuu moja. Ukijaribu kuangalia vyama vilivyo vingi vya wafanyakazi vinaundwa na wanachama walio wengi na wanaotoka katika mashirika mengi amabyo ni ya kifaida zaidi kwa mfano viwanda, makampuni ya uchimbaji madini, mafunta, makampuni ya utalii, kilimo, uvuvi, ufugaji, n.k. Sisi kaka ASIZE (NGO's), sifa zetu kubwa na kuu ni kwamba sisi sio mashirika ya kiserikali, sio mashirika ya kutengeneza faida za kifedha, sio mashirka ya kidini, sio mashirika ya kisiasa, nk. hivyo ni vyema kuwa na chombo chetu kitakachofanania na sifa hizi ili kiweze kujali maslahi yetu kwa kuzingatia misingi. ASIZE zilizo nyingi zimesajiliwa na zian wafanyakazi ambao hulipa kodi kwa serikali (PAYE), hivyo hata kama tutkakjuwa chini ya TUCTA ingekuwa ni jambo la busara kuwa na chombo chetu kwanza ambacho kingeweza kufanya uwakilishi wa kiusahaihi katika chombo chochote cha kutetea haki za wafanyakazi kilichopo ngazi ya taifa na kimataifa. Naunga mkono hoja ya kuwanzishwa kwa umoja wa wafanyakazi wa ASIZE. Michael Mpombo, Moshi. Michael Mpombo, Moshi 12/05/2010
    Jukumu la kulea watoto yatima wa Tanzania ni la watanzania wote kwa ujumla kimsingi. Jambo hili kwasasa limebaki tu kinadharia maana kivitendo jukumu hili limeachiwa kwa asasi za kiraia ambazo misaada yake mingi huipata si kutoka kwa watanzania wenyewe bali kwa wageni wanaotoka inje ya Tanzania.Ndugu, jamaa, marafiki na jamii ya kitanzania ya watoto yatima kwa hivi sasa imebaki na mtizamo kuwa jukumu hili si lao tena bali ni la mashirika ya kuhudumia watoto yatima ambapo kiukweli jamii ya kitanzania inachangia kwa kiasi kidogo sana katika malezi ya watoto hawa hata wawapo kwenye vituo vya watoto yatima. Huu ni mtizamo wa jamii yetu ambao haujengi hata kidogo juu ya muafaka wa nani anawajibika na tatizo hili. Jukumu hili ni letu wote sisi watanzania. Tunajitia aibu kwa kuendelea kutegema misaada toka wageni katika malezi ya watoto yatima. Jamii yote kwa ujumla kuanzia ngazi ya familia, ukoo, kitongoji, kijiji/mtaa, kata, tarafa, wilaya, mkoa na taifa inawajibika na jambo hili moja kwa moja. Lakini je tunalifahamu hilo na tupo tayari kuwajibika na hilo!Hata tukiwa tayari na uwajibikaji, je ni kwa kiwango gani!Serikali moja kwa moja inawajibika na suala hili kwani kila raia wa inchi hii ana haki sawa na mwingine na anapaswa kupata fursa sawa na mwingine. Kwa watoto yatima ambao tunategemea baadae ndio watakaokuwa wazalishaji wazuri na kulipatia taifa pato la kutosha, serikali inpaswa kuwasaidia pindi wanapokuwa hawana mtu wa kuwasaidia. Kimsingi kila mzazi anawajibika na mtoto wake, kwa watoto yatima ni kwamba wazazi wao wote wamekufa au mzazi mmoja amekufa, hivyo watoto hawa hawana ungalizi wa kutosha na kuendelezwa. Naomba, serikali ikishirikiana na familia, ndugu, jamaa na marafiki wa watoto yatima kuwajibika na hili. Ninapotamka serikali siamanishi serikali kuu tuu, ni serikali kuanzia ngazi ya kitongoji, mtaa, kijiji, kata, n.k Ninaamini kuwa taifa lolote hapa duniani, haliwezi kuendelea vizuri kama litarithiwa na raia wake ambao hawana ujuzi na uelewa/ufahamu wowote katika kukabiliana na changamoto zozote za kiuchumi. kisiasa, kijamii, n.k. Kama tunataka taifa letu lizidi kuendelea tunahitaji kuwekeza kwa watoto wetu maana ndio watakaokuwa wakala wa maendeleo ya taifa letu. Yatima ni miongoni mwa watoto ambao nao wanahitaji kulirithi taifa lao ili wazidi kuliendeleza kwa manufaa ya jamii yote kwa ujumla. Nasema jukumu la kulea watoto yatima wa Tanzania ni letu sisi watanzania, tukianzia ngazi ya familia, ukoo, kitongoji na hadi ngazi ya taifa. Tubadilike, tutumie rasilimali tulizonazo kufanya chochote tuwezacho kuhakikisha watoto hawa wanasaidika. Asante,Michael Mpombo, Kili Centre. Michael Mpombo, KILI CENTRE, MOSHI. 05/05/2010
    Ni kweli asasi zetu za kiraia zinashindwa kujiendesha kwa sababu zinategema mno ruzuku kwa asilimia mia moja na ruzuku hizi zilizo nyingi hazitoki Tanzania bali zinatoka kwa wahsani mbalimbali waliopo inje ya inchi. Wahsani hawa wanaotupatia sisi ruzuku ili kuendesha shughuli zetu za asasi mabalimbali za kiraia na kwaajili ya kuleta maendeleo chanya kwa watanzania wenzetu, huwa na malengo yao binafsi ambayo kwa watu wa kawaida tu hawawezi kugundua kuwa yanaendeleza kukua kwa umaskini wetu. Ruzuku wanazotupatia wahsani hawa ukiangalia mara nyingi hulenga maslahi yao zaidi kuliko maslahi ya walengwa katika mradi wa aina yoyote. Sikatai kuwa wapo wachache (wahsani) ambao huwa ni washirika wa kweli katika kuleta maendeleo yetu lakini walio wengi hutusaidia ili tuendelee kuwa maskini na wazidi kututawala kifikra,kiuchumi, kisiasa, kijamii, n.k. Asasi za kiraia hapa Tanzania zilizo nyingi haziwezi kupunguza umaskini wa watanzania kwa sababu zenyewe hazina mikakati mathubuti ya kuanzisha miradi ambayo itawaingizia vipato ambavyo watavitumia katika tutekeleza shughuli zao za maendeleo kwa raia. Ruzuku tupewazo na wahsani zina masharti lukuki ambayo kwa namna moja au nyingine ni unyanyasaji wa kifikra kwa sababu ili upate ruzuku ya kwao ni laazima uimbe wimbo wao na uzungumze lugha yao pasipo kujali kuwa na sisi tuna wimbo wetu na lugha yetu. Ili tuweze kuimba wimbo wetu na kuzungumza lugha yetu ni laazima tuwe na mikakati ya maksudi ya kuwa na vianzo vyetu vya ndani vya kujipatia ruzuku. Ni vizuri kwa serikali kutenga budget kwaajili ya kuzisaidia asasi za kiraia kutekeleza majukumu yake maana kila litekelezwalo na asasi yoyote ya kiraia ilipaswa kutekelewa na serikali, hivyo si mbaya kwa serikali kufanya asasi kuwa wakala wake wa kutekeleza baadhi ya shughuli ambazo ilipaswa kuzitekeleza. Vile vile tuwe na miradi ya kuzalisha sisi kama asasi za kiraia ili tusitegemee kwa asilimia mia moja kutekeleza shughuli zetu kwa kupitia ruzuku za wahsani, Asante, Michael Mpombo, Kili Centre. Michael Mpombo, Kili Centre, Moshi. 05/05/2010
    Featured Topic: |
    NINI KINAFUATA ZANZIBAR?
    Useful Links
  • Others
  • Regional and global civil society networks
  • National civil society networks and organizations
  • CSO Directory
  • cso websites funded
    by fcs
  • Morogoro paralegal Centre
  • Christian Council Of Tanzania
  • Guluka Kwalala Youth Environmental Group
  • Agenda Participation 2000
  • About Us | contact us | Press Room | Vacancies | Privacy Policy | Terms and Conditions | Join our mailing list | Webmail
    © 2009 - 2012 The Foundation for Civil Society. All Rights Reserved.